Sura

  1. 1
  2. 2
  3. 3
  4. 4
  5. 5

Agano la Kale

Agano Jipya

Maombolezo 5 Biblia Habari Njema (BHN)

Kuomba huruma

1. Ukumbuke ee Mwenyezi-Mungu, mambo yaliyotupata!Utuangalie, uone jinsi tulivyoaibishwa!

2. Nchi yetu imekabidhiwa wageni,nyumba zetu watu wengine.

3. Tumekuwa yatima, bila baba,mama zetu wameachwa kama wajane.

4. Maji yetu tunayapata kwa fedha,kuni zetu kwa kuzinunua.

5. Tunalazimishwa kufanya kazi kama punda,tumechoka lakini haturuhusiwi kupumzika.

6. Wamisri na Waashuru tumewanyoshea mikono,ili tupate chakula cha kutosha.

7. Wazee wetu walitenda dhambi na hawapo tena;nasi tunateseka kwa sababu ya makosa yao.

8. Watumwa ndio wanaotutawala,wala hakuna wa kutuokoa mikononi mwao.

9. Chakula chetu twapata kwa kuhatarisha maisha yetu,maana wauaji wanazurura huko mashambani.

10. Ngozi zetu zawaka moto kama tanurikwa sababu ya njaa inayotuchoma.

11. Wanawake wetu wanashikwa kwa nguvu mjini Siyoni,binti zetu katika vijiji vya Yuda.

12. Wakuu wetu wametungikwa kwa mikono yao;wazee wetu hawapewi heshima yoyote.

13. Vijana wanalazimishwa kusaga nafaka kwa mawe,wavulana wanayumbayumba kwa mizigo ya kuni.

14. Wazee wameacha kutoa mashauri yao,vijana wameacha kuimba.

15. Furaha ya mioyo yetu imetoweka,ngoma zetu zimegeuzwa kuwa ombolezo.

16. Fahari tuliyojivunia imetokomea.Ole wetu kwa kuwa tumetenda dhambi!

17. Kwa ajili hiyo tumeugua moyoni,kwa mambo hayo macho yetu yamefifia.

18. Maana mlima Siyoni umeachwa tupu,mbweha wanazurura humo.

19. Lakini wewe Mwenyezi-Mungu watawala milele,utawala wako wadumu vizazi vyote.

20. Mbona umetuacha muda mrefu hivyo?Mbona umetutupa siku nyingi hivyo?

21. Uturekebishe ee Mwenyezi-Mungu, nasi tukurudie,uturudishie fahari yetu kama zamani.

22. Au, je, umetukataa kabisa?Je, umetukasirikia mno?