1. Ukumbuke ee Mwenyezi-Mungu, mambo yaliyotupata!Utuangalie, uone jinsi tulivyoaibishwa!
2. Nchi yetu imekabidhiwa wageni,nyumba zetu watu wengine.
3. Tumekuwa yatima, bila baba,mama zetu wameachwa kama wajane.
4. Maji yetu tunayapata kwa fedha,kuni zetu kwa kuzinunua.
5. Tunalazimishwa kufanya kazi kama punda,tumechoka lakini haturuhusiwi kupumzika.