Sura

  1. 1
  2. 2
  3. 3
  4. 4
  5. 5

Agano la Kale

Agano Jipya

Maombolezo 2 Biblia Habari Njema (BHN)

Adhabu ya Yerusalemu

1. Mwenyezi-Mungu, kwa hasira yake,amewaweka watu wa Siyoni gizani.Fahari ya Israeli ameibwaga chini.Siku ya hasira yakealilitupilia mbali hata hekalu lake.

2. Mwenyezi-Mungu ameharibu bila hurumamakazi yote ya wazawa wa Yakobo.Kwa ghadhabu yake amezibomoa ngome za watu wa Yuda.Ufalme wao na watawala wakeameuporomosha chini kwa aibu.

3. Nguvu yote ya Israeli ameivunja kwa hasira.Hakunyosha mkono kuwasaidiawalipokutana na adui;amewawakia watu wa Yakobo kama moto,akateketeza kila kitu.

4. Amevuta upinde wake kama adui,na kuuweka mkono wake wa kulia tayari,amewaua wote tuliowaonea faharikatika maskani yetu watu wa Siyoni.Ametumiminia hasira yake kama moto.

5. Mwenyezi-Mungu amekuwa kama adui,ameangamiza watu wa Israeli;majumba yake yote ameyaharibu,ngome zake amezibomoa.Amewazidishia watu wa Yudamatanga na maombolezo.

6. Hekalu lake amelibomoa kama kitalu bustanini,maskani yake ameiharibu.Amefutilia mbali sikukuu na Sabato huko Siyoni,kwa hasira yake kuu amewakataa mfalme na makuhani.

7. Mwenyezi-Mungu ameipuuza madhabahu yakena hekalu lake amelikataa.Kuta za majumba mjini amewaachia maadui wazibomoe,wakapiga kelele humo nyumbani kwa Mwenyezi-Mungukama kelele za wakati wa sikukuu.

8. Mwenyezi-Mungu alipania kuubomoa ukuta wa mji wa Siyoni;aliupima na kuhakikisha kila kitu kimeharibiwa;minara na kuta za nje ya mji akazifanya ukiwa,zote kwa pamoja zikaangamia.

9. Malango yake yameanguka chini,makomeo yake ameyaharibu na kuyavunjavunja.Mfalme na wakuu wake wako uhamishoni kati ya mataifa.Mwongozo wa sheria umetoweka kabisa,manabii wake hawapati tena maonokutoka kwake Mwenyezi-Mungu.

10. Wazee wa Siyoni wameketi chini kimya,wamejitia mavumbi vichwanina kuvaa mavazi ya gunia.Wasichana wa Yerusalemu wameinamisha vichwa.

11. Macho yangu yamevimba kwa kulia,roho yangu imechafuka.Moyo wangu una huzuni nyingikwa sababu ya kuangamizwa kwa watu wangukwa sababu watoto wachanga wanazirai katika barabara za mji.

12. Wanawalilia mama zao:“Wapi chakula, wapi kinywaji?”Huku wanazirai kama majeruhikatika barabara za mjini,na kukata roho mikononi mwa mama zao.

13. Nikuambie nini ee Yerusalemu?Nikulinganishe na nini?Nikufananishe na kitu ganiili niweze kukufariji,ee Siyoni uliye mzuri?Maafa yako ni mengi kama bahari.Ni nani awezaye kukuponya?

14. Manabii wako wamekuonea maono madanganyifu,hawakufichua wazi uovu wakoili wapate kukurekebisha,bali walikuonea kauli ya uongo na ya kupotosha.

15. Wapita njia wote wanakudhihaki;wanakuzomea, ee Yerusalemu,wakitikisa vichwa vyao kwa dharau na kusema:“Je, huu ndio ule mji uliofikia upeo wa uzuri,mji uliokuwa furaha ya dunia nzima?”

16. Maadui zako wote wanakuzomea,wanakufyonya na kukusagia meno,huku wakisema, “Tumemwangamiza!Kweli, siku ile tuliyoingojea kwa hamusasa imefika na tumeiona!”

17. Mwenyezi-Mungu amefanya yale aliyokusudia,ametekeleza yale aliyotishia;kama alivyopanga tangu kaleameangamiza bila huruma yoyote;amewafanya maadui wafurahie adhabu yako,amewakuza mashujaa wa maadui zako.

18. Kuta zako, ee mji wa Siyoni, zimlilie Mwenyezi-Mungu!Machozi na yatiririke kama mto mchana na usiku!Lia na kuomboleza bila kupumzika!

19. Usiku kucha uamkeamke ukalie.Mfungulie Mwenyezi-Mungu yaliyo moyoni mwako.Mwinulie mikono yako kuwaombea watoto wako,watoto wanaozirai kwa njaa popote barabarani.

20. Tazama ee Mwenyezi-Mungu uone!Je, kuna yeyote uliyemtendea ulivyotutendea sisi?Je, hata kina mama wawale watoto wao?Je, nao makuhani wauawe hekaluni mwako?

21. Maiti za vijana na wazee zimelala vumbini barabarani,wasichana na wavulana wangu wameuawa kwa upanga;umewaua bila huruma siku ya hasira yako.

22. Umewaalika kama kwenye sikukuumaadui zangu walionitisha kila upande.Katika siku ya hasira yako ee Mwenyezi-Mungu,hakuna aliyetoroka au kunusurika.Wale niliowazaa na kuwaleaadui zangu wamewaangamiza.