Agano la Kale

Agano Jipya

Maombolezo 2:3-7 Biblia Habari Njema (BHN)

3. Nguvu yote ya Israeli ameivunja kwa hasira.Hakunyosha mkono kuwasaidiawalipokutana na adui;amewawakia watu wa Yakobo kama moto,akateketeza kila kitu.

4. Amevuta upinde wake kama adui,na kuuweka mkono wake wa kulia tayari,amewaua wote tuliowaonea faharikatika maskani yetu watu wa Siyoni.Ametumiminia hasira yake kama moto.

5. Mwenyezi-Mungu amekuwa kama adui,ameangamiza watu wa Israeli;majumba yake yote ameyaharibu,ngome zake amezibomoa.Amewazidishia watu wa Yudamatanga na maombolezo.

6. Hekalu lake amelibomoa kama kitalu bustanini,maskani yake ameiharibu.Amefutilia mbali sikukuu na Sabato huko Siyoni,kwa hasira yake kuu amewakataa mfalme na makuhani.

7. Mwenyezi-Mungu ameipuuza madhabahu yakena hekalu lake amelikataa.Kuta za majumba mjini amewaachia maadui wazibomoe,wakapiga kelele humo nyumbani kwa Mwenyezi-Mungukama kelele za wakati wa sikukuu.

Kusoma sura kamili Maombolezo 2