Agano la Kale

Agano Jipya

Maombolezo 2:17-22 Biblia Habari Njema (BHN)

17. Mwenyezi-Mungu amefanya yale aliyokusudia,ametekeleza yale aliyotishia;kama alivyopanga tangu kaleameangamiza bila huruma yoyote;amewafanya maadui wafurahie adhabu yako,amewakuza mashujaa wa maadui zako.

18. Kuta zako, ee mji wa Siyoni, zimlilie Mwenyezi-Mungu!Machozi na yatiririke kama mto mchana na usiku!Lia na kuomboleza bila kupumzika!

19. Usiku kucha uamkeamke ukalie.Mfungulie Mwenyezi-Mungu yaliyo moyoni mwako.Mwinulie mikono yako kuwaombea watoto wako,watoto wanaozirai kwa njaa popote barabarani.

20. Tazama ee Mwenyezi-Mungu uone!Je, kuna yeyote uliyemtendea ulivyotutendea sisi?Je, hata kina mama wawale watoto wao?Je, nao makuhani wauawe hekaluni mwako?

21. Maiti za vijana na wazee zimelala vumbini barabarani,wasichana na wavulana wangu wameuawa kwa upanga;umewaua bila huruma siku ya hasira yako.

22. Umewaalika kama kwenye sikukuumaadui zangu walionitisha kila upande.Katika siku ya hasira yako ee Mwenyezi-Mungu,hakuna aliyetoroka au kunusurika.Wale niliowazaa na kuwaleaadui zangu wamewaangamiza.

Kusoma sura kamili Maombolezo 2