Agano la Kale

Agano Jipya

Maombolezo 1:2-8 Biblia Habari Njema (BHN)

2. Walia usiku kucha;machozi yautiririka.Hakuna hata mmoja wa wapenzi wake wa kuufariji.Rafiki zake wote wameuhadaa;wote wamekuwa adui zake.

3. Watu wa Yuda wamekwenda uhamishonipamoja na mateso na utumwa mkali.Sasa wanakaa miongoni mwa watu wa mataifa,wala hawapati mahali pa kupumzika.Waliowafuatia wamewakamata wakiwa taabuni.

4. Barabara za kwenda Siyoni zinasikitisha;hakuna wapitao kwenda kwenye sikukuu.Malango ya mji wa Siyoni ni tupu;makuhani wake wanapiga kite,wasichana wake wana huzuni,na mji wenyewe uko taabuni.

5. Adui zake ndio wanaoutawala na wanafanikiwa,kwani Mwenyezi-Mungu ameutesakwa sababu ya makosa mengi.Watoto wake wametekwa na kupelekwa mbali.

6. Fahari yote ya watu wa Siyoni imewatoweka;wakuu wake wamekuwa kama kulungu wasio na malisho.Bila nguvu waliwakimbia watesi wao.

7. Ukiwa sasa magofu matupu,Yerusalemu wakumbuka fahari yake.Ulipoangukia mikononi mwa maadui zake,hakuna aliyekuwako kuusaidia.Washindi wake walichekelea kuanguka kwake.

8. Yerusalemu ulitenda dhambi mbaya,ukawa mchafu kwa dhambi zake.Wote waliousifia wanaudharau,maana wameuona uchi wake.Wenyewe wapiga kite na kujificha kwa aibu.

Kusoma sura kamili Maombolezo 1