Agano la Kale

Agano Jipya

Kutoka 7:21-25 Biblia Habari Njema (BHN)

21. Samaki wakafa, mto ukanuka vibaya sana hata Wamisri wasiweze kunywa maji yake. Nchi nzima ikajaa damu.

22. Lakini wachawi wa Misri kwa kutumia uchawi wao wakafanya vivyo hivyo. Kwa hiyo moyo wa Farao ukabaki kuwa mgumu, naye hakuwasikiliza Mose na Aroni; ikawa kama Mwenyezi-Mungu alivyokuwa amesema.

23. Basi, Farao akarudi nyumbani kwake, na hata haya yaliyotokea hakuyajali.

24. Wamisri wote wakachimbachimba kandokando ya mto Nili ili wapate maji ya kunywa, kwani hawakuweza kunywa maji ya mto huo.

25. Pigo hilo la mto Nili lilidumu siku saba.

Kusoma sura kamili Kutoka 7