Agano la Kale

Agano Jipya

Kutoka 6:1-5 Biblia Habari Njema (BHN)

1. Lakini Mwenyezi-Mungu akamjibu Mose, “Sasa utaona jinsi nitakavyomtenda Farao; maana kwa nguvu atalazimika kuwaacha watu wangu watoke. Naam, kwa nguvu atawafukuza waondoke nchini mwake.”

2. Mungu akamwambia Mose, “Mimi ni Mwenyezi-Mungu.

3. Nilimtokea Abrahamu, Isaka na Yakobo nikijulikana kama Mungu Mwenye Nguvu, ingawa kwa jina langu, Mwenyezi-Mungu, sikuwajulisha.

4. Tena nilifanya agano nao kwamba nitawapa nchi ya Kanaani ambako waliishi kama wageni.

5. Zaidi ya hayo, nimesikia kilio cha Waisraeli ambao wamelazimishwa kufanya kazi za kitumwa na Wamisri, nikalikumbuka agano langu.

Kusoma sura kamili Kutoka 6