Agano la Kale

Agano Jipya

Kutoka 23:6-11 Biblia Habari Njema (BHN)

6. “Usiipotoshe haki anayostahili maskini katika kesi yake.

7. Jitenge mbali na mashtaka ya uongo wala usiwaue wasio na hatia na waadilifu, maana mimi sitamsamehe mtu mwovu.

8. Usipokee rushwa, maana rushwa huwapofusha wakuu na kupotosha mambo ya wenye haki.

9. “Usimdhulumu mgeni; nyinyi mwajua hali ya kuwa mgeni, maana mlikuwa wageni nchini Misri.

10. “Kwa muda wa miaka sita utapanda mashamba yako na kuvuna mazao yake.

11. Lakini mnamo mwaka wa saba, utayaacha mashamba yako bila kupanda mbegu, ili maskini miongoni mwa watu wako wapate chakula kilichosalia humo, na wanyama wa porini wale. Utafanya vivyo hivyo katika shamba lako la mizabibu na la mizeituni.

Kusoma sura kamili Kutoka 23