1. “Usitoe habari za uongo. Usishirikiane na mtu mwovu ili kuwa shahidi mbaya.
2. Usifuate genge la watu kutenda uovu, wala usijumuike na genge la watu kutoa ushahidi mahakamani ili kupotosha haki.
3. Usiwe na upendeleo katika kesi ya maskini.
4. “Ukimkuta ng'ombe au punda wa adui yako amepotea, utamrudishia mwenyewe.
5. Ukimwona punda wa mtu anayekuchukia ameanguka na mzigo wake, msaidie mtu huyo kumsimamisha punda wake, wala usimwache na kwenda zako.
6. “Usiipotoshe haki anayostahili maskini katika kesi yake.