Agano la Kale

Agano Jipya

Kumbukumbu La Sheria 7:1-3 Biblia Habari Njema (BHN)

1. “Mwenyezi-Mungu, Mungu wenu, atawafikisha kwenye nchi ambayo mtakwenda kufanya makao yenu na atayafukuza mataifa mengi kutoka nchi hiyo. Mtakapoingia, atayafukuza mbele yenu mataifa saba makubwa na yenye nguvu kuliko nyinyi: Wahiti, Wagirgashi, Waamori, Wakanaani, Waperizi, Wahivi na Wayebusi.

2. Pia, baada ya Mwenyezi-Mungu, Mungu wenu, kuyatia mikononi mwenu, mkawashinda watu hao na kuwaangamiza kabisa, msifanye agano lolote nao wala msiwahurumie.

3. Msioane nao, wala msiwaoze binti zenu au wana wenu kwao.

Kusoma sura kamili Kumbukumbu La Sheria 7