Agano la Kale

Agano Jipya

Kumbukumbu La Sheria 33:6-12 Biblia Habari Njema (BHN)

6. Mose alisema juu ya kabila la Reubeni:“Reubeni aishi wala asife,na watu wake wasiwe wachache.”

7. Juu ya kabila la Yuda alisema:“Ee Mwenyezi-Mungu usikilize kilio cha kabila la Yuda;umrudishe tena kwa watu wale wengine.Upigane kwa mikono yako kwa ajili yake,ulisaidie kabila la Yuda dhidi ya adui zake.”

8. Juu ya kabila la Lawi, alisema:“Ee Mwenyezi-Mungu ulipatie Lawi kauli yako ya Urimu,kauli yako ya thumimu kwa hao waaminifu wako,ambao uliwajaribu huko Masa.

9. Ulishindana nao kwenye maji ya Meriba.Walawi walioamua kuwaacha wazee wao,wakawasahau jamaa zao,wasiwatambue hata watoto waomaana walizingatia amri zako,na kushika agano lako.

10. Na wawafundishe wazawa wa Yakobo maagizo yako;wawafundishe watu wa Israeli sheria yako.Walawi na wafukize ubani mbele yako,sadaka nzima za kuteketezwa madhabahuni pako.

11. Ee Mwenyezi-Mungu, uzibariki nguvu zao,uzikubali kazi za mikono yao;uzivunjilie mbali nguvu za maadui zao,nguvu za wanaowachukia hata wasiinuke tena.”

12. Juu ya kabila la Benyamini alisema:“Hili ni kabila alipendalo Mwenyezi-Mungu,nalo hukaa salama karibu naye.Yeye hulilinda mchana kutwa,na kukaa kati ya milima yake.”

Kusoma sura kamili Kumbukumbu La Sheria 33