30. Mtu mmoja anawezaje kuwashinda watu 1,000,au watu wawili wanawezaje kuwashinda watu 10,000,isipokuwa kama Mwamba wao amewatupa,Mwenyezi-Mungu wao amewaacha?
31. Hata adui zetu wenyewe wamekiri wazi,mwamba wao hauna nguvu kama mwamba wetu.
32. Maana mizabibu yao ni miche ya Sodomazimetoka katika konde za Gomora;zabibu zake ni zabibu zenye sumu,vishada vyake ni vichungu.
33. Divai yao ni kama sumu ya nyoka,ina sumu kali ya majoka.