Sura

  1. 1
  2. 2
  3. 3
  4. 4
  5. 5
  6. 6
  7. 7
  8. 8
  9. 9
  10. 10
  11. 11
  12. 12
  13. 13
  14. 14
  15. 15
  16. 16
  17. 17
  18. 18
  19. 19
  20. 20
  21. 21
  22. 22
  23. 23
  24. 24
  25. 25
  26. 26
  27. 27
  28. 28
  29. 29
  30. 30
  31. 31
  32. 32
  33. 33
  34. 34

Agano la Kale

Agano Jipya

Kumbukumbu La Sheria 32 Biblia Habari Njema (BHN)

1. “Tegeni masikio enyi mbingu:Sikiliza, ee dunia, maneno ninayosema.

2. Mafundisho yangu na yatone kama mvua,maneno yangu yadondoke kama umande,kama manyunyu kwenye mimea michanga,kama mvua nyepesi katika majani mabichi.

3. Maana nitalitangaza jina la Mwenyezi-Mungu,nanyi mseme, ‘Mungu wetu ni Mkuu’.

4. “Mwenyezi-Mungu ni Mwamba wa usalama;kazi zake ni kamilifu,njia zake zote ni za haki.Yeye ni Mungu mwaminifu asiye na kosa,yeye hufanya mambo ya uadilifu na ya haki.

5. Lakini nyinyi mmekosa uaminifu kwake,nyinyi sio watoto wake tena kwa sababu ya uovu,nyinyi ni kizazi kiovu na kipotovu.

6. Mnawezaje kumlipa hivyo Mwenyezi-Mungu,enyi watu wapumbavu na msio na akili?Je, yeye siye Baba yenu aliyewaumba,aliyewafanya na kuwaimarisha?

7. Kumbukeni siku zilizopita,fikirieni miaka ya vizazi vingi;waulizeni baba zenu nao watawajulisha,waulizeni wakubwa wenu nao watawaeleza.

8. Mungu Mkuu alipoyagawia mataifa mali yao,alipowagawa wanadamu,kila taifa alilipatia mipaka yake,

9. kulingana na idadi ya watoto wa Mungu,lakini alijiwekea watu wa Yakobo kuwa wake,hao alijichagulia kuwa mali yake.

10. Aliwakuta katika nchi ya jangwa,nyika tupu zenye upepo mkali.Aliwalinda na kuwatunza,aliwafanya kama mboni ya jicho lake.

11. Kama tai alindaye kiota chake,na kurukaruka juu ya makinda yake,akitandaza mabawa yake ili kuwashikilia,na kuwabeba juu ya mabawa yake.

12. Yeye Mwenyezi-Mungu mwenyewe aliwaongozana hapakuwa na mungu mwingine wa kumsaidia.

13. Aliwapitisha katika nyanda za juu za nchi,nao wakala mazao ya mashambani.Akawapa asali miambani waonjena mafuta kutoka mwamba mgumu.

14. Aliwapa siagi na maziwa ya mifugo,mafuta ya wanakondoo na kondoo madume,makundi ya mifugo ya Bashani na mbuzi.Aliwapa ngano nzuri kabisa na divai mpya wakanywa.

15. Watu wa Israeli walinona na kupiga mateke;walinenepa, wakawa na kitambi na kunawiri;kisha wakamwacha Mungu aliyewaumba,wakamdharau Mwamba wa wokovu wao.

16. Walimfanya aone wivu mkali kwa miungu yao,walimchochea akasirike kwa matendo yao ya kuchukiza.

17. Walitambikia majini ambayo hayakuwa miungu,waliiendea miungu ambayo hawakuijua kamwe,miungu mipya iliyotokea siku za karibuni,ambayo wazee wao hawakuiheshimu kamwe.

18. Hamkumjali Mwamba aliyewapa uhai,mlimsahau Mungu aliyewazaa nyinyi.

19. Mwenyezi-Mungu aliona jambo hilo akawaacha;aliwakataa watoto wake, waume kwa wake.

20. Akasema, ‘Nitawaficha uso wangunione mwisho wao utakuwaje!Maana wao ni kizazi kipotovu,watoto wasio na uaminifu wowote.

21. Wamenichochea kuona wivu kwa kitu kisicho mungu,wamenikasirisha kwa sanamu zao.Hivyo nitawafanya waone wivu kwa kisicho watu,nitawakasirisha kwa kutumia taifa la wapumbavu.

22. Hasira yangu imewaka moto,inachoma mpaka chini kuzimu,itateketeza dunia na vilivyomo,itaunguza misingi ya milima.

23. Nitarundika maafa chungu nzima juu yao,nitawamalizia mishale yangu.

24. Watakonda kwa njaa,wataangamizwa kwa homa kali.Nitapeleka wanyama wenye meno makali kuwashambulia,na nyoka wenye sumu wanaotambaa mavumbini.

25. Vita vitasababisha vifo vingi njena majumbani hofu itawatawala,vijana wa kiume na wa kike watauawahata wanyonyao na wazee wenye mvi.

26. Nilisema, ningaliwaangamiza kabisana kuwafanya wasikumbukwe tena na mtu yeyote,

27. ila tu kwa sababu ya majivuno ya maadui zaoili maadui zao wasije wakafikiria vingine;wasije wakasema, wamefaulu kuwaangamiza,nami Mwenyezi-Mungu sihusiki katika mambo haya!’

28. “Israeli ni taifa lisilo na akili,watu wake hawana busara ndani yao.

29. Wangekuwa na hekima wangejua kwa nini walishindwa,wangeweza kuelewa mwisho wao utakuwaje.

30. Mtu mmoja anawezaje kuwashinda watu 1,000,au watu wawili wanawezaje kuwashinda watu 10,000,isipokuwa kama Mwamba wao amewatupa,Mwenyezi-Mungu wao amewaacha?

31. Hata adui zetu wenyewe wamekiri wazi,mwamba wao hauna nguvu kama mwamba wetu.

32. Maana mizabibu yao ni miche ya Sodomazimetoka katika konde za Gomora;zabibu zake ni zabibu zenye sumu,vishada vyake ni vichungu.

33. Divai yao ni kama sumu ya nyoka,ina sumu kali ya majoka.

34. “Je sina njia ya kuwaadhibu?Silaha zangu ninazo mkononi.

35. Kisasi ni juu yangu,mimi nitalipiza,wakati miguu yao itakapoteleza;maana siku yao ya maafa imewadia,mwisho wao u karibu sana.

36. Mwenyezi-Mungu atawatetea watu wake,na kuwahurumia watumishi wake,wakati atakapoona nguvu zao zimeishia,wala hakuna aliyebaki, mfungwa au mtu huru.

37. Ndipo Mwenyezi-Mungu atakapowauliza watu wake,‘Iko wapi ile miungu yenu,mwamba mlioukimbilia usalama?’

38. Iko wapi hiyo miungu iliyokula matoleo yenuna kunywa divai na tambiko zenu za kinywaji?Basi na iinuke, iwasaidieni;acheni hiyo iwe kinga yenu sasa!

39. Oneni kuwa mimi ndimi Munguna wala hakuna mwingine ila mimi.Mimi huua na kuweka hai;hujeruhi na kuponya,na hakuna awezaye kumwokoa yeyote mikononi mwangu.

40. Nanyosha mkono wangu mbinguni,na kuapa, kwa uhai wangu wa milele,

41. kama mkiuona upanga wangu umeremetao,na kunyosha mkono kutoa hukumu,nitawalipiza kisasi maadui zangu,nitawaadhibu wale wanaonichukia.

42. Mishale yangu nitailevya kwa damu,upanga wangu utashiba nyama,utalowa damu ya majeruhi na matekana adui wenye nywele ndefu.

43. “Enyi mataifa washangilieni watu wake,maana yeye hulipiza kisasi damu ya watumishi wake,huwalipiza kisasi wapinzani wake,na kuitakasa nchi ya watu wake.”

44. Mose alikuja mbele ya Yoshua, mwana wa Nuni, wakakariri maneno ya wimbo huu, ili Waisraeli wote wausikie.

Wosia wa Mose

45. Mose alipomaliza kuwaambia watu wa Israeli maneno haya yote,

46. aliwaambia, “Yawekeni mioyoni mwenu maneno yote ambayo ninawapeni leo. Lazima muwaamuru watoto wenu ili wafuate kwa uaminifu maneno yote ya sheria hii.

47. Maana sheria hii si maneno matupu bali ni uhai wenu; kwa sheria hii mtaishi maisha marefu katika nchi mnayokwenda kuimiliki, ngambo ya mto Yordani.”

48. Siku hiyohiyo, Mwenyezi-Mungu akamwambia Mose,

49. “Panda mlima huu wa Abarimu, mlima Nebo katika nchi ya Moabu, mkabala wa mji Yeriko, ukaiangalie nchi ya Kanaani ninayowapa Waisraeli waimiliki.

50. Kisha ufariki hukohuko mlimani kama kaka yako Aroni alivyofariki katika mlima Hori,

51. kwa sababu nyote wawili mlivunja uaminifu wenu kwangu mbele ya Waisraeli mlipokuwa kwenye maji ya Meriba, karibu na mji wa Kadeshi, katika jangwa la Sini, mkakosa kuuthibitisha utakatifu wangu kati ya Waisraeli.

52. Utaiona nchi iliyo mbele yako, lakini hutaingia katika nchi hiyo ninayowapa Waisraeli.”