Agano la Kale

Agano Jipya

Kumbukumbu La Sheria 32:23-33 Biblia Habari Njema (BHN)

23. Nitarundika maafa chungu nzima juu yao,nitawamalizia mishale yangu.

24. Watakonda kwa njaa,wataangamizwa kwa homa kali.Nitapeleka wanyama wenye meno makali kuwashambulia,na nyoka wenye sumu wanaotambaa mavumbini.

25. Vita vitasababisha vifo vingi njena majumbani hofu itawatawala,vijana wa kiume na wa kike watauawahata wanyonyao na wazee wenye mvi.

26. Nilisema, ningaliwaangamiza kabisana kuwafanya wasikumbukwe tena na mtu yeyote,

27. ila tu kwa sababu ya majivuno ya maadui zaoili maadui zao wasije wakafikiria vingine;wasije wakasema, wamefaulu kuwaangamiza,nami Mwenyezi-Mungu sihusiki katika mambo haya!’

28. “Israeli ni taifa lisilo na akili,watu wake hawana busara ndani yao.

29. Wangekuwa na hekima wangejua kwa nini walishindwa,wangeweza kuelewa mwisho wao utakuwaje.

30. Mtu mmoja anawezaje kuwashinda watu 1,000,au watu wawili wanawezaje kuwashinda watu 10,000,isipokuwa kama Mwamba wao amewatupa,Mwenyezi-Mungu wao amewaacha?

31. Hata adui zetu wenyewe wamekiri wazi,mwamba wao hauna nguvu kama mwamba wetu.

32. Maana mizabibu yao ni miche ya Sodomazimetoka katika konde za Gomora;zabibu zake ni zabibu zenye sumu,vishada vyake ni vichungu.

33. Divai yao ni kama sumu ya nyoka,ina sumu kali ya majoka.

Kusoma sura kamili Kumbukumbu La Sheria 32