Agano la Kale

Agano Jipya

Kumbukumbu La Sheria 32:22-38 Biblia Habari Njema (BHN)

22. Hasira yangu imewaka moto,inachoma mpaka chini kuzimu,itateketeza dunia na vilivyomo,itaunguza misingi ya milima.

23. Nitarundika maafa chungu nzima juu yao,nitawamalizia mishale yangu.

24. Watakonda kwa njaa,wataangamizwa kwa homa kali.Nitapeleka wanyama wenye meno makali kuwashambulia,na nyoka wenye sumu wanaotambaa mavumbini.

25. Vita vitasababisha vifo vingi njena majumbani hofu itawatawala,vijana wa kiume na wa kike watauawahata wanyonyao na wazee wenye mvi.

26. Nilisema, ningaliwaangamiza kabisana kuwafanya wasikumbukwe tena na mtu yeyote,

27. ila tu kwa sababu ya majivuno ya maadui zaoili maadui zao wasije wakafikiria vingine;wasije wakasema, wamefaulu kuwaangamiza,nami Mwenyezi-Mungu sihusiki katika mambo haya!’

28. “Israeli ni taifa lisilo na akili,watu wake hawana busara ndani yao.

29. Wangekuwa na hekima wangejua kwa nini walishindwa,wangeweza kuelewa mwisho wao utakuwaje.

30. Mtu mmoja anawezaje kuwashinda watu 1,000,au watu wawili wanawezaje kuwashinda watu 10,000,isipokuwa kama Mwamba wao amewatupa,Mwenyezi-Mungu wao amewaacha?

31. Hata adui zetu wenyewe wamekiri wazi,mwamba wao hauna nguvu kama mwamba wetu.

32. Maana mizabibu yao ni miche ya Sodomazimetoka katika konde za Gomora;zabibu zake ni zabibu zenye sumu,vishada vyake ni vichungu.

33. Divai yao ni kama sumu ya nyoka,ina sumu kali ya majoka.

34. “Je sina njia ya kuwaadhibu?Silaha zangu ninazo mkononi.

35. Kisasi ni juu yangu,mimi nitalipiza,wakati miguu yao itakapoteleza;maana siku yao ya maafa imewadia,mwisho wao u karibu sana.

36. Mwenyezi-Mungu atawatetea watu wake,na kuwahurumia watumishi wake,wakati atakapoona nguvu zao zimeishia,wala hakuna aliyebaki, mfungwa au mtu huru.

37. Ndipo Mwenyezi-Mungu atakapowauliza watu wake,‘Iko wapi ile miungu yenu,mwamba mlioukimbilia usalama?’

38. Iko wapi hiyo miungu iliyokula matoleo yenuna kunywa divai na tambiko zenu za kinywaji?Basi na iinuke, iwasaidieni;acheni hiyo iwe kinga yenu sasa!

Kusoma sura kamili Kumbukumbu La Sheria 32