Agano la Kale

Agano Jipya

Kumbukumbu La Sheria 20:8-14 Biblia Habari Njema (BHN)

8. Maofisa wataendelea kuwaambia watu, ‘Je, yupo hapa mtu aliyekufa moyo? Arudi nyumbani, asije akasababisha wenzake kufa moyo kama yeye.’

9. Maofisa wakisha sema na watu, basi makamanda watawaongoza watu.

10. “Mnapokaribia mji kuushambulia, kwanza wapeni wakazi wake masharti ya amani.

11. Wakazi wa mji huo wakitaka amani na kujisalimisha kwenu, basi watu wote waliomo humo watawatumikieni na kufanya kazi za kulazimishwa.

12. Lakini wakazi wa mji huo wasipofanya amani nanyi, lakini wakapigana vita nanyi, basi, mtauzingira mji wao;

13. naye Mwenyezi-Mungu, Mungu wenu akiutia mikononi mwenu, mtawaua kwa upanga wanaume wote;

14. lakini wanawake na watoto, ng'ombe, na vyote vilivyomo mjini, nyara zake zote mwaweza kuchukua mateka kwa ajili yenu wenyewe; mnaweza kufurahia nyara za adui zenu, ambazo Mwenyezi-Mungu, Mungu wenu, amewapa.

Kusoma sura kamili Kumbukumbu La Sheria 20