Agano la Kale

Agano Jipya

Isaya 9:4-15 Biblia Habari Njema (BHN)

4. Maana nira nzito walizobeba,nira walizokuwa wamefungwa,na fimbo ya wanyapara wao,umezivunjavunja kama wakati wa Wamidiani.

5. Viatu vyote vya washambulizi vitanina mavazi yote yenye madoa ya damuyatateketezwa kama kuni za kuwasha moto.

6. Maana mtoto amezaliwa kwa ajili yetu,tumepewa mtoto wa kiume.Naye atapewa mamlaka ya kutawala.Ataitwa: “Mshauri wa Ajabu”.“Mungu Mwenye Nguvu”,“Baba wa Milele”,“Mfalme wa Amani”.

7. Utawala wake utastawi daima,amani ya ufalme wake haitakoma.Atachukua wadhifa wa mfalme Daudina kutawala juu ya ufalme wake;ataustawisha na kuuimarisha,kwa haki na uadilifu,tangu sasa na hata milele.Hayo atayafanya Mwenyezi-Mungu wa majeshi.

8. Mwenyezi-Mungu ametoa tamko dhidi ya Yakobonalo litampata Israeli.

9. Watu wote watatambua,ukoo wote wa Efraimuna wakazi wa Samaria.Kwa kiburi na majivuno wanasema:

10. “Kuta za matofali zimeangukalakini sisi tutazijenga kwa mawe yaliyochongwa!Nyumba za boriti za mikuyu zimeharibiwalakini mahali pake tutajenga za mierezi.”

11. Basi, Mwenyezi-Mungu atawaletea wapinzanina kuwachochea maadui zao.

12. Waaramu upande wa mashariki,Wafilisti upande wa magharibi,wamepanua vinywa vyao kuimeza Israeli.Hata hivyo, hasira yake haijatulia,bado ameunyosha mkono wake.

13. Ingawa aliwaadhibu watu,hawakumrudia Mwenyezi-Mungu wa majeshi.

14. Basi kwa muda wa siku moja tu,Mwenyezi-Mungu atakata katika Israeli vichwa na mikia,tawi la mtende na nyasi:

15. Vichwa ndio wazee na waheshimiwa,mikia ndio manabii wafundishao uongo.

Kusoma sura kamili Isaya 9