Agano la Kale

Agano Jipya

Isaya 9:17-21 Biblia Habari Njema (BHN)

17. Kwa hiyo, Mwenyezi-Mungu hawahurumii vijana wao,hana huruma juu ya yatima na wajane wao;kwani hakuna hata mmoja amchaye Mungu,kila mtu husema uongo.Hata hivyo, hasira yake haijatulia,bado ameunyosha mkono wake.

18. Uovu huwaka kama motouteketezao mbigili na miiba;huwaka kama moto msituni,na kutoa moshi mzito upandao angani juu.

19. Kwa ghadhabu ya Mwenyezi-Mungu wa majeshinchi imechomwa moto,na watu ni kama kuni za kuuwasha.Hakuna mtu anayemhurumia ndugu yake;

20. wananyanganya upande mmoja na hawatosheki;wanakula upande mwingine lakini hawashibi.Kila mmoja anamshambulia mwenzake.

21. Manase dhidi ya Efraimu,Efraimu dhidi ya Manasena wote wawili dhidi ya Yuda.Hata hivyo, hasira ya Mwenyezi-Mungu haijatulia,bado ameunyosha mkono wake.

Kusoma sura kamili Isaya 9