Agano la Kale

Agano Jipya

Isaya 9:1-10 Biblia Habari Njema (BHN)

1. Lakini nchi ile iliyokuwa imekumbwa na huzuni haitabaki daima katika giza hilo kuu. Hapo awali Mungu alizifedhehesha nchi za Zebuluni na Naftali, lakini siku za usoni ataifanikisha sehemu hii ya baharini na nchi iliyo ngambo ya Yordani na hata Galilaya wanamoishi watu wa mataifa.

2. Watu waliotembea gizaniwameona mwanga mkubwa.Watu walioishi katika nchi ya giza kuu,sasa mwanga umewaangazia.

3. Wewe, ee Mungu, umelikuza taifa,umeiongeza furaha yake.Watu wanafurahi mbele yako,wana furaha kama wakati wa mavuno,kama wafurahivyo wanaogawana nyara.

4. Maana nira nzito walizobeba,nira walizokuwa wamefungwa,na fimbo ya wanyapara wao,umezivunjavunja kama wakati wa Wamidiani.

5. Viatu vyote vya washambulizi vitanina mavazi yote yenye madoa ya damuyatateketezwa kama kuni za kuwasha moto.

6. Maana mtoto amezaliwa kwa ajili yetu,tumepewa mtoto wa kiume.Naye atapewa mamlaka ya kutawala.Ataitwa: “Mshauri wa Ajabu”.“Mungu Mwenye Nguvu”,“Baba wa Milele”,“Mfalme wa Amani”.

7. Utawala wake utastawi daima,amani ya ufalme wake haitakoma.Atachukua wadhifa wa mfalme Daudina kutawala juu ya ufalme wake;ataustawisha na kuuimarisha,kwa haki na uadilifu,tangu sasa na hata milele.Hayo atayafanya Mwenyezi-Mungu wa majeshi.

8. Mwenyezi-Mungu ametoa tamko dhidi ya Yakobonalo litampata Israeli.

9. Watu wote watatambua,ukoo wote wa Efraimuna wakazi wa Samaria.Kwa kiburi na majivuno wanasema:

10. “Kuta za matofali zimeangukalakini sisi tutazijenga kwa mawe yaliyochongwa!Nyumba za boriti za mikuyu zimeharibiwalakini mahali pake tutajenga za mierezi.”

Kusoma sura kamili Isaya 9