Agano la Kale

Agano Jipya

Isaya 65:7-17 Biblia Habari Njema (BHN)

7. Mimi Mwenyezi-Mungu, nitawalipiza maovu yaowayalipie na maovu ya wazee wao.Wao waliifukizia ubani miungu yao milimani,wakanitukana mimi huko vilimani.Nitawafanya walipe kwa wingi,watayalipia matendo yao ya awali.”

8. Mwenyezi-Mungu asema hivi:“Mtu akikuta kishada cha zabibu nzuri,watu husema: ‘Tusikiharibu; kina baraka.’Ndivyo nitakavyofanya kwa ajili ya watumishi wangu;sitawaangamiza wote.

9. Nitawajalia watu wa Yakobo,na Yuda nitamjalia warithi wa milima yangu;watumishi wangu watakaa huko.

10. Nchi tambarare ya Sharoni itakuwa malisho,bonde la Akori litakuwa mapumziko ya mifugokwa ajili ya watu wangu walionitafuta.

11. “Lakini nitafanya nini na nyinyimnaoniacha mimi Mwenyezi-Mungu,msioujali Siyoni, mlima wangu mtakatifu,nyinyi mnaoabudu mungu ‘Gadi’,na kumtolea tambiko ya divai mungu ‘Meni’?

12. Nimewapangia kifo kwa upanga,nyote mtaangukia machinjoni!Maana, nilipowaita, hamkuniitikia;niliponena, hamkunisikiliza.Mlitenda yaliyo maovu mbele yangu,mkachagua yale nisiyoyapenda.

13. Basi, mimi Mwenyezi-Mungu nasema,watumishi wangu watakula,lakini nyinyi mtaona njaa;watumishi wangu watakunywa,lakini nyinyi mtaona kiu;watumishi wangu watafurahi,lakini nyinyi mtafedheheka.

14. Watumishi wangu wataimba kwa furaha moyoni,lakini nyinyi mtalia kwa uchungu moyonina kupiga kelele kwa uchungu mkubwa rohoni.

15. Wale niliowachagua nitawapa jina jipya.Lakini nyinyi jina lenu watalitumia kulaania;‘Watasema: Bwana Mungu awaue kama hao.’

16. Basi, mwenye kujitakia baraka nchini,atajitakia baraka kwa Mungu wa kweli.Mwenye kuapa katika nchi hii,ataapa kwa Mungu wa kweli.Maana taabu za zamani zimepitazimetoweka kabisa mbele yangu.

17. “Sasa, naumba mbingu mpya na dunia mpya.mambo ya zamani hayatakumbukwa tena.

Kusoma sura kamili Isaya 65