Agano la Kale

Agano Jipya

Isaya 65:18-21 Biblia Habari Njema (BHN)

18. Furahini, mkashangilie milele,kwa ajili ya vitu hivi ninavyoumba.Yerusalemu nitaufanya mji wa shangwe,na watu wake watu wenye furaha.

19. Nami nitaufurahia mji wa Yerusalemu,nitawafurahia watu wangu.Sauti ya kilio haitasikika tena,kilio cha taabu hakitakuwako.

20. Hakutakuwa tena na vifo vya watoto wachanga,wazee nao hawatakufa kabla ya wakati wao.Akifa mtu wa miaka 100 amekufa akiwa kijana;na akifa kabla ya miaka 100 ni balaa.

21. Watu watajenga nyumba na kuishi humo;watalima mizabibu na kula matunda yake.

Kusoma sura kamili Isaya 65