Agano la Kale

Agano Jipya

Isaya 6:10-13 Biblia Habari Njema (BHN)

10. Kisha akaniambia,“Zipumbaze akili za watu hawa,masikio yao yasisikie,macho yao yasione;ili wasije wakaona kwa macho yao,wakasikia kwa masikio yao,wakaelewa kwa akili zao,na kunigeukia, nao wakaponywa.”

11. Mimi nikauliza,“Bwana, mpaka lini?”Naye akanijibu,“Mpaka hapo miji itakapobaki tupu bila wakazi,nyumba bila watu,na nchi itakapoharibiwa kabisa.

12. Nami Mwenyezi-Mungu nitawapeleka watu mbali,na kuifanya nchi yote kuwa mahame.

13. Hata wakibaki watu asilimia kumi,nao pia watateketezwa.Hao watakuwa kama mvinje au mwaloniambao kisiki chake kimebaki baada ya kukatwa.”(Kisiki hicho ni mbegu takatifu ya chanzo kipya.)

Kusoma sura kamili Isaya 6