Agano la Kale

Agano Jipya

Isaya 57:3-14 Biblia Habari Njema (BHN)

3. Lakini Mwenyezi-Mungu asema:“Njoni hapa nyinyi wana wa wachawi;nyinyi wazawa wa wachawi, wazinzi na malaya.

4. Je, mnadhani mnamdhihaki nani?Mnamfyonya nani na kumtolea ulimi?Nyinyi wenyewe ni wahalifu tangu mwanzo,nyinyi ni kizazi kidanganyifu.

5. Nyinyi mnawaka tamaa kwenye miti ya mialoni,na katika kila mti wa majani mabichi.Mnawachinja watoto wenuna kuwatambika katika mabonde na nyufa za majabali.

6. Mnachagua mawe laini mabondeni,na kuyafanya kitovu cha maisha yenu.Mnayamiminia tambiko ya kinywajina kuyapelekea tambiko ya nafaka!Je, mimi nitaridhishwa kwa vitu hivyo?

7. Mmeweka vitanda vyenu juu ya milima mikubwa,na kwenda huko kutoa tambiko.

8. Nyuma ya milango na miimommetundika kinyago chenu.Nyinyi mnaniacha mimina kutandika na kuvipanua vitanda vyenu.Mnafanya mapatano na hao mliopenda vitanda vyao.Humo mnazitosheleza tamaa zenu mbaya,huku mnakodolea macho kinyago chenu.

9. Mnajitia marashi na manukato kwa wingikisha mnakwenda kumwabudu Moleki.Mnawatuma wajumbe wenu huko na huko,kujitafutia miungu ya kuabudu;hata kuzimu walifika.

10. Mlichoshwa na safari zenu ndefu,hata hivyo hamkukata tamaa;mlijipatia nguvu mpya,ndiyo maana hamkuzimia.

11. “Mlimwogopa na kutishwa na nanihata mkasema uongo,mkaacha kunikumbuka mimina kuacha kabisa kunifikiria?Mimi sikuwaambia kitu kwa muda mrefu;ndio maana labda mkaacha kuniheshimu!

12. Mnafikiri mnafanya sawa,lakini nitayafichua matendo yenu,nayo miungu yenu haitawafaa kitu.

13. Mtakapolia kuomba msaada,rundo la vinyago vyenu na liwaokoe!Upepo utavipeperushia mbali;naam, pumzi itavitupilia mbali.Lakini watakaokimbilia usalama kwangu,wataimiliki nchi,mlima wangu mtakatifu utakuwa mali yao.”

14. Mwenyezi-Mungu asema hivi:“Jengeni! Jengeni! Tayarisheni njia!Ondoeni vikwazo vyote njiani mwa watu wangu!”

Kusoma sura kamili Isaya 57