Agano la Kale

Agano Jipya

Isaya 57:10-21 Biblia Habari Njema (BHN)

10. Mlichoshwa na safari zenu ndefu,hata hivyo hamkukata tamaa;mlijipatia nguvu mpya,ndiyo maana hamkuzimia.

11. “Mlimwogopa na kutishwa na nanihata mkasema uongo,mkaacha kunikumbuka mimina kuacha kabisa kunifikiria?Mimi sikuwaambia kitu kwa muda mrefu;ndio maana labda mkaacha kuniheshimu!

12. Mnafikiri mnafanya sawa,lakini nitayafichua matendo yenu,nayo miungu yenu haitawafaa kitu.

13. Mtakapolia kuomba msaada,rundo la vinyago vyenu na liwaokoe!Upepo utavipeperushia mbali;naam, pumzi itavitupilia mbali.Lakini watakaokimbilia usalama kwangu,wataimiliki nchi,mlima wangu mtakatifu utakuwa mali yao.”

14. Mwenyezi-Mungu asema hivi:“Jengeni! Jengeni! Tayarisheni njia!Ondoeni vikwazo vyote njiani mwa watu wangu!”

15. Hivi ndivyo asemavyo Mungu aliye juu kabisa,aishiye milele na ambaye jina lake ni “Mtakatifu”:“Mimi nakaa huko juu, mahali patakatifu,nakaa pia na wenye majuto na wanyenyekevu.Mimi nitawatia moyo walio wanyenyekevuna kuwapa nguvu wenye majuto.

16. Maana sitaendelea kuwalaumuwala kuwakasirikia daima.La sivyo hao niliowaumba watadhoofika mbele yangu,nami ndiye niliyewapa pumzi yangu ya uhai.

17. Niliwakasirikia kwa sababu ya uovu na tamaa zao;niliwaadhibu, nikauficha uso wangu na kukasirika.Lakini wao waliendelea kufuata njia zao wenyewe.

18. Niliiona mienendo yao, lakini nitawaponya;nitawaongoza na kuwapa faraja,nitawatuliza hao wanaoomboleza.

19. Mimi nitawapa amani,amani kwa walio mbali na walio karibu!Mimi nitawaponya.

20. Lakini waovu ni kama bahari iliyochafuka,ambayo haiwezi kutulia;mawimbi yake hutupa tope na takataka.”

21. Mungu wangu asema hivi:“Watu waovu sitawapa amani.”

Kusoma sura kamili Isaya 57