Agano la Kale

Agano Jipya

Isaya 55:3-11 Biblia Habari Njema (BHN)

3. “Tegeni sikio enyi watu wangu, mje kwangu;nisikilizeni, ili mpate kuishi.Nami nitafanya nanyi agano la milele;nitawapeni fadhili nilizomwahidi Daudi.

4. Mimi nilimfanya kiongozi na kamanda wa mataifaili yeye anishuhudie kwa watu wa mataifa.

5. Sasa utayaita mataifa usiyoyajua,watu wa mataifa yasiyokutambua watakujia mbio,kwa sababu yangu mimi Mwenyezi-Mungu, Mungu wako;kwa sababu yangu mimi Mtakatifu wa Israeliniliyekufanya wewe utukuke.”

6. Mtafuteni Mwenyezi-Mungu wakati bado anapatikana,mwombeni msaada wakati yupo bado karibu.

7. Waovu na waache njia zao mbaya,watu wabaya waachane na mawazo yao mabaya;wamrudie Mwenyezi-Mungu apate kuwahurumia,wamwendee Mungu wetu maana atawasamehe.

8. Maana, Mwenyezi-Mungu asema hivi:“Mawazo yangu si kama mawazo yenu,wala njia zangu si kama njia zenu.

9. Kama vile mbingu zilivyo mbali na dunia,ndivyo njia zangu zilivyo mbali na zenu,na mawazo yangu mbali na mawazo yenu.

10. “Kama vile mvua na theluji ishukavyo toka mbinguni,wala hairudi huko bali huinywesha ardhi,ikaifanya ichipue mimea ikakua,ikampatia mpanzi mbegu na kuwapa watu chakula,

11. vivyo hivyo na neno langu mimi:Halitanirudia bila mafanikio,bali litatekeleza matakwa yangu,litafanikiwa lengo nililoliwekea.

Kusoma sura kamili Isaya 55