Agano la Kale

Agano Jipya

Isaya 55:1-7 Biblia Habari Njema (BHN)

1. “Haya! Kila mwenye kiu na aje kwenye maji!Njoni, nyote hata msio na fedha;nunueni ngano mkale,nunueni divai na maziwa.Bila fedha, bila gharama!

2. Mbona mnatumia fedha yenukwa ajili ya kitu kisicho chakula?Ya nini kutoa jasho lenu kwa kitu kisichoshibisha?Nisikilizeni mimi kwa makini,nanyi mtakula vilivyo bora,na kufurahia vinono.

3. “Tegeni sikio enyi watu wangu, mje kwangu;nisikilizeni, ili mpate kuishi.Nami nitafanya nanyi agano la milele;nitawapeni fadhili nilizomwahidi Daudi.

4. Mimi nilimfanya kiongozi na kamanda wa mataifaili yeye anishuhudie kwa watu wa mataifa.

5. Sasa utayaita mataifa usiyoyajua,watu wa mataifa yasiyokutambua watakujia mbio,kwa sababu yangu mimi Mwenyezi-Mungu, Mungu wako;kwa sababu yangu mimi Mtakatifu wa Israeliniliyekufanya wewe utukuke.”

6. Mtafuteni Mwenyezi-Mungu wakati bado anapatikana,mwombeni msaada wakati yupo bado karibu.

7. Waovu na waache njia zao mbaya,watu wabaya waachane na mawazo yao mabaya;wamrudie Mwenyezi-Mungu apate kuwahurumia,wamwendee Mungu wetu maana atawasamehe.

Kusoma sura kamili Isaya 55