Agano la Kale

Agano Jipya

Isaya 53:1-4 Biblia Habari Njema (BHN)

1. Nani aliyeamini mambo tuliyosikia?Nani aliyetambua kuwa mkono wa Mwenyezi-Mungu ulihusika?

2. Maana, mbele yake Mwenyezi-Mungu,mtumishi wake alikua kama mti mchanga,kama mzizi katika nchi kavu.Hakuwa na umbo wala sura ya kutupendeza,wala hakuwa na uzuri wowote wa kutuvutia.

3. Alidharauliwa na kukataliwa na watu,alikuwa mtu wa uchungu na huzuni.Alikuwa kama mtu kinyaa kwa watu;alidharauliwa na tukamwona si kitu.

4. Hata hivyo alivumilia majonzi yetu,na kubeba huzuni zetu.Sisi tulifikiri amepata adhabu,amepigwa na Mungu na kuteswa.

Kusoma sura kamili Isaya 53