Agano la Kale

Agano Jipya

Isaya 49:2-13 Biblia Habari Njema (BHN)

2. Aliyapa ukali maneno yangu kama upanga mkali,alinificha katika kivuli cha mkono wake;aliufanya ujumbe wangu mkali kama ncha ya mshale,akanificha katika podo lake.

3. Aliniambia, “Wewe ni mtumishi wangu;kwako, Israeli, watu watanitukuza.”

4. Lakini mimi nikafikiri,“Nimeshughulika bure,nimetumia nguvu zangu bure kabisa.”Hata hivyo, Mwenyezi-Mungu atanipa haki yangu;tuzo la kazi yangu liko kwa Mungu.

5. Lakini asema sasa Mwenyezi-Mungu,ambaye aliniita tangu tumboni mwa mama yanguili nipate kuwa mtumishi wake;nilirudishe taifa la Yakobo kwake,niwakusanye wazawa wa Israeli kwake.Mwenyezi-Mungu amenijalia heshima mbele yake.Mungu wangu amekuwa ndiye nguvu yangu.

6. Yeye asema: “Haitoshi tu wewe kuwa mtumishi wangu,uyainue makabila ya Yakobo,na kurekebisha watu wa Israeli waliobaki.Nitakufanya uwe mwanga wa mataifa,niwaletee wokovu watu wote duniani.”

7. Mwenyezi-Mungu, Mkombozi na Mtakatifu wa Israeli,amwambia hivi yule anayedharauliwa mno,yule anayechukiwa na mataifa,na ambaye ni mtumishi wa watawala:“Wafalme watakuona nao watasimama kwa heshima,naam, wakuu watainama na kukusujudiakwa sababu yangu mimi Mwenyezi-Munguambaye hutimiza ahadi zangu;kwa sababu yangu mimi Mtakatifu wa Israeliambaye nimekuteua wewe.”

8. Mwenyezi-Mungu asema hivi:“Wakati wa kufaa nilikujibu ombi lako;wakati wa wokovu nilikusaidia.Nimekuweka na kukufanyauwe kiungo cha agano langu na mataifa yote:Kuirekebisha nchi iliyoharibika,na kuwarudishia wenyewe ardhi hiyo;

9. kuwaambia wafungwa, ‘Tokeni humo gerezani’,na wale walio gizani, ‘Njoni nje mwangani!’Kila mahali watakapokwenda watapata chakulahata kwenye vilima vitupu watapata malisho.

10. Hawataona tena njaa wala kuwa na kiu.Upepo wa hari wala jua havitawachoma,mimi niliyewahurumia nitawaongozana kuwapeleka kwenye chemchemi za maji.

11. Milima yote nitaifanya kuwa njia,na barabara zangu kuu nitazitengeneza.

12. Watu wangu watarudi kutoka mbali,wengine kutoka kaskazini na magharibi,wengine kutoka upande wa kusini.”

13. Imbeni kwa furaha, enyi mbingu!Shangilia ewe dunia.Pazeni sauti mwimbe enyi milima,maana Mwenyezi-Mungu amewafariji watu wake,naam, atawaonea huruma watu wake wanaoteseka.

Kusoma sura kamili Isaya 49