Agano la Kale

Agano Jipya

Isaya 48:3-8 Biblia Habari Njema (BHN)

3. “Nilitangaza zamani matukio ya awali,niliyatamka mimi mwenyewena kuyafanya yajulikane kwenu.Mara nikaanza kuyatekeleza,nayo yakapata kutukia.

4. Lakini nilikujua wewe kuwa mkaidi;kichwa kigumu kama chuma,uso wako mkavu kama shaba.

5. Kwa hiyo nilikutangazia tangu zamani,kabla hayajatukia mimi nilikutangazia,usije ukasema, ‘Kinyago changu kiliyatenda hayo,sanamu zangu za kuchonga na kusubu ziliyafanya.’

6. “Wewe uliyasikia na sasa unayaona yote.Kwa nini huwezi kuyakiri?Tangu sasa nitakujulisha mambo mapya;mambo yaliyofichika ambayo hukuyajua.

7. Mambo hayo yanatukia sasa;hukupata kuyasikia kabla ya leo,hivyo huwezi kusema, ‘Aa! Nilikwisha yajua.’

8. Hujapata kamwe kuyasikia wala kuyajua;tangu zamani masikio yako hayakuyasikia.Nilijua kuwa wewe ni mwenye hila,na kwamba wewe ni mwasi tangu kuzaliwa.

Kusoma sura kamili Isaya 48