Agano la Kale

Agano Jipya

Isaya 48:14-22 Biblia Habari Njema (BHN)

14. “Kusanyikeni nyote msikilize!Nani kati ya miungu yenu aliyetabiri vitu hivi?Mimi Mwenyezi-Mungu nampenda Koreshi;yeye atatekeleza lengo langu kuhusu Babuloni,naam, yeye atawashambulia Wakaldayo.

15. Mimi, naam, mimi nimeyasema na kumwita;nimemleta, naye atafaulu katika mpango wake.

16. Njoni karibu nami msikie jambo hili:Tangu mwanzo mimi sikusema kwa siri,tangu mambo hayo yaanze kutendeka, nimekuwapo.”Sasa, Bwana Mungu amenituma,na kunipa nguvu ya roho yake.

17. Mwenyezi-Mungu, Mtakatifu wa Israeli,Mkombozi wako, asema hivi:“Mimi ndimi Mwenyezi-Mungu, Mungu wako,ninayekufundisha kwa faida yako,ninayekuongoza katika njia unayotakiwa kwenda.

18. Laiti ungalizitii amri zangu!Hapo baraka zingekutiririkia kama mto,ungepata fanaka kwa wingi kama mawimbi ya bahari.

19. Wazawa wako wangekuwa wengi kama mchanga,naam, wangekuwa wengi kama chembe za mchanga.Jina lao kamwe lisingaliondolewa,kumbukumbu lao halingalitoweka mbele yangu.”

20. Sasa, ondokeni Babuloni!Kimbieni kutoka Kaldayo!Tangazeni jambo hili kwa sauti za shangwe,enezeni habari zake kila mahali duniani.Semeni: “Mwenyezi-Mungu amelikomboataifa la mtumishi wake Yakobo.”

21. Alipowaongoza jangwani hawakuona kiu,aliwatiririshia maji kutoka mwambani,aliupasua mwamba maji yakabubujika.

22. Lakini Mwenyezi-Mungu asema hivi:“Watu waovu sitawapa amani.”

Kusoma sura kamili Isaya 48