1. Sikilizeni, enyi watu wa Yakobo,enyi mnaojulikana kwa jina la Israeli,nyinyi mlio wa ukoo wa Yuda.Nyinyi huapa kwa jina la Mwenyezi-Mungu,na kudai mnamwabudu Mungu wa Israeli;lakini hayo si ukweli wala sawa.
2. Nyinyi mnaona fahari kujiita watu wa mji mtakatifu,na kujidai kumtegemea Mungu wa Israeli,ambaye jina lake ni Mwenyezi-Mungu wa majeshi.
3. “Nilitangaza zamani matukio ya awali,niliyatamka mimi mwenyewena kuyafanya yajulikane kwenu.Mara nikaanza kuyatekeleza,nayo yakapata kutukia.
4. Lakini nilikujua wewe kuwa mkaidi;kichwa kigumu kama chuma,uso wako mkavu kama shaba.
5. Kwa hiyo nilikutangazia tangu zamani,kabla hayajatukia mimi nilikutangazia,usije ukasema, ‘Kinyago changu kiliyatenda hayo,sanamu zangu za kuchonga na kusubu ziliyafanya.’