Agano la Kale

Agano Jipya

Isaya 47:1-7 Biblia Habari Njema (BHN)

1. “Teremka uketi mavumbiniewe Babuloni binti mzuri!Keti chini pasipo kiti cha enziewe binti wa Wakaldayo!Tokea sasa hutaitwa tena mwororo wala nadhifu.

2. Twaa mawe ya kusagia, usage unga kama mtumwa!Vua utaji wako, ukavue na mavazi yako!Pandishia vazi lako miguuni, ukavuke mito.

3. Watu watauona uchi wako;naam, wataiona aibu yako.Mimi nitalipiza kisasi,wala sitamhurumia yeyote.”

4. Mkombozi wetu ndiye Mtakatifu wa Israeli;Mwenyezi-Mungu wa majeshi ndilo jina lake.

5. Mwenyezi-Mungu asema:“Ewe taifa la Wakaldayolililo kama binti mzuri,keti kimya na kutokomea gizani.Maana umepoteza hadhi yakoya kuwa bimkubwa wa falme.

6. Niliwakasirikia watu wangu Israeli,nikawafanya watu wangu kuwa haramu.Niliwatia mikononi mwako,nawe hukuwaonea huruma;na wazee uliwatwisha nira nzito mno.

7. Ulijisemea moyoni: ‘Nitakuwa malkia milele’,nawe hukuyatafakari mambo yanayotokea,wala kufikiri mwisho wake.

Kusoma sura kamili Isaya 47