Agano la Kale

Agano Jipya

Isaya 45:1-12 Biblia Habari Njema (BHN)

1. Mwenyezi-Mungu asema hivi juu ya Koreshi:“Wewe ni mfalme wangu niliyekuteua;mimi naitegemeza nguvu yakoili uyashinde mataifa mbele yako,na kuzivunja nguvu za wafalme.Mimi nayafungua malango ya mji mbele yako,na hakuna lango litakalofungwa.

2. Mimi nitakutangulia,na kuisawazisha milima mbele yako.Nitaivunjavunja milango ya shaba,na kuvikatakata vizuizi vyake vya chuma.

3. Nitakupa hazina zilizofichwa gizani,na mali iliyo mahali pa siri,upate kutambua kwamba mimi ndimi Mwenyezi-Mungu,Mungu wa Israeli, ninayekuita kwa jina lako.

4. Kwa ajili ya mtumishi wangu Yakobo,naam, kwa ajili ya mteule wangu Israeli,nimekuita kwa jina lako;nimekupa jina la heshima ingawa wewe hunijui.

5. “Mimi ni Mwenyezi-Mungu, wala hakuna mwingine;hakuna Mungu mwingine ila mimi.Ninakuimarisha ingawa wewe hunijui,

6. ili watu wote, toka mashariki hadi magharibi,wajue kwamba hakuna Mungu mwingine ila mimi;mimi ni Mwenyezi-Mungu na hakuna mwingine.

7. Mimi hufanya mwanga na kuumba giza;huleta fanaka na kusababisha balaa.Mimi Mwenyezi-Mungu hutenda vitu hivi vyote.

8. Enyi mbingu, nyesheni kutoka huko juu,mawingu na yadondoshe uadilifu;dunia na ifunuke, ichipushe wokovu,na kuchanusha uadilifu pia!Mimi, Mwenyezi-Mungu nimefanya hayo.”

9. Ole wake mtu ashindanaye na Muumba wake,mtu aliye chombo cha udongokushindana na mfinyanzi wake!Je, udongo humwuliza anayeufinyanga:“Unatengeneza nini hapa?”Au kumwambia, “Kazi yako si kamili!”

10. Ole wake mtoto amwambiaye baba yake,“Kwa nini umenizaa?”Au amwambiaye mama yake,“Ya nini umenileta duniani?”

11. Mwenyezi-Mungu, Mtakatifu wa Israeli,Mungu, Muumba wa Israeli asema:“Je, mwathubutu kuniuliza juu ya watoto wangu,au kuniamuru juu ya kazi zangu mwenyewe?

12. Ni mimi niliyeifanya dunia,na kuumba binadamu aishiye humo.Mikono yangu ndiyo iliyozitandaza mbingu,na jeshi lote la nyota liko kwa amri yangu.

Kusoma sura kamili Isaya 45