Agano la Kale

Agano Jipya

Isaya 44:21-28 Biblia Habari Njema (BHN)

21. Mwenyezi-Mungu asema hivi:“Ewe taifa la Yakobo kumbuka;naam, kumbuka ewe Israeli:Wewe ni mtumishi wangu.Nilikuumba ili uwe mtumishi wangu,nami kamwe sitakusahau.

22. Nimeyafagilia mbali makosa yako kama wingu,nimezifanya dhambi zako zitoweke kama ukungu.Rudi kwangu maana mimi nimekukomboa.”

23. Imbeni kwa furaha enyi mbingu,kwa sababu ya hayo aliyotenda Mwenyezi-Mungu.Pazeni sauti enyi vilindi vya dunia!Imbeni kwa furaha enyi milima!Enyi misitu na miti yote iliyomo, imbeni.Maana Mwenyezi-Mungu amewakomboa wazawa wa Yakobo,naye atatukuka katika nchi ya Israeli.

24. Mwenyezi-Mungu, Mkombozi wako,aliyekuumba tangu tumboni mwa mama yako, asema:“Mimi ndimi Mwenyezi-Mungu niliyeumba vitu vyote.Mimi peke yangu nilizitandaza mbingu,niliiumba dunia kwa nguvu yangu mwenyewe!

25. Mimi huzivuruga ishara za watabiri waongona kuwapumbaza waaguzi.Mimi huyakanusha maneno ya wenye hekimana kufanya ujuzi wao kuwa upumbavu.

26. Lakini huuthibitisha ujumbe wa mtumishi wangu,na kukamilisha maaguzi ya wajumbe wangu.Mimi ndimi niuambiaye mji wa Yerusalemu:Wewe Yerusalemu, utakaliwa tena na watu.Na miji ya Yuda:Nyinyi mtajengeka tena:Magofu yenu nitayarekebisha tena.

27. Mimi ndimi ninayeviamuru vilindi:Kaukeni.

28. Ndimi nimwambiaye Koreshi:Wewe utawachunga watu kwa niaba yangu.Wewe utatekeleza mipango yangu yote.Ndimi ninayesema kuhusu Yerusalemu:Wewe Yerusalemu utajengwa tena upya;na juu ya hekalu: Msingi wako utawekwa tena.”

Kusoma sura kamili Isaya 44