Agano la Kale

Agano Jipya

Isaya 42:2-19 Biblia Habari Njema (BHN)

2. Hatalia wala hatapiga kelele,wala hatapaza sauti yake barabarani.

3. Mwanzi uliochubuka hatauvunja,utambi ufukao moshi hatauzima;ataleta haki kwa uaminifu.

4. Yeye hatafifia wala kufa moyo,hata atakapoimarisha haki duniani.Watu wa mbali wanangojea mwongozo wake.”

5. Hivi ndivyo asemavyo Mwenyezi-Mungualiyeziumba mbingu, akazitandaza kama hema,yeye aliyeiunda nchi na vyote vilivyomo,yeye awapaye watu waliomo pumzi,na kuwajalia uhai wote waishio humo:

6. “Mimi Mwenyezi-Mungu nimekuita kutenda haki,nimekushika mkono na kukulinda.Kwa njia yako nitaweka ahadi na watu wote,wewe utakuwa mwanga wa mataifa.

7. Utayafumbua macho ya vipofu,utawatoa wafungwa gerezani,waliokaa gizani utawaletea uhuru.

8. Jina langu mimi ni Mwenyezi-Mungu;utukufu wangu sitampa mwingine,wala sifa zangu sanamu za miungu.

9. Tazama, mambo niliyotabiri yametukia;na sasa natangaza mambo mapya,nakueleza hayo kabla hayajatukia.”

10. Mwimbieni Mwenyezi-Mungu wimbo mpya!Dunia yote iimbe sifa zake:Bahari na vyote vilivyomo,nchi za mbali na wakazi wake;

11. jangwa na miji yake yote ipaaze sauti,vijiji vya wakazi wa Kedari vimsifu,wakazi wa Sela waimbe kwa shangwe;wapaaze sauti kutoka mlimani juu.

12. Wote wakaao nchi za mbali,na wamtukuze na kumsifu Mwenyezi-Mungu.

13. Mwenyezi-Mungu ajitokeza kama shujaa;kama askari vitani ajikakamua kupigana.Anapaza sauti kubwa ya vita,na kujionesha mwenye nguvu dhidi ya maadui zake.

14. Mwenyezi-Mungu asema hivi:“Kwa muda mrefu sasa nimenyamaza,nimekaa kimya na kujizuia;lakini sasa nitalia kama mama anayejifungua,anayetweta pamoja na kuhema.

15. Nitaharibu milima na vilima,na majani yote nitayakausha.Mito ya maji nitaigeuza kuwa nchi kavu,na mabwawa ya maji nitayakausha.

16. “Nitawaongoza vipofu katika njia wasiyoifahamu,nitawaongoza katika njia ambazo hawazijui.Mbele yao giza nitaligeuza kuwa mwanga,na mahali pa kuparuza patakuwa laini.Huo ndio mpango wangu wa kufanya,nami nitautekeleza.

17. Wote wanaotegemea sanamu za miungu,wote wanaoziambia: Nyinyi ni miungu yetu;watakomeshwa na kuaibishwa.

18. “Sikilizeni enyi viziwi!Tazameni enyi vipofu, mpate kuona!

19. Nani aliye kipofu ila mtumishi wangu?Nani aliye kiziwi kama mjumbe ninayemtuma?Ni nani aliye kipofu kama huyu niliyemweka wakfu,au kipofu kama mtumishi wa Mwenyezi-Mungu?

Kusoma sura kamili Isaya 42