Agano la Kale

Agano Jipya

Isaya 41:4-11 Biblia Habari Njema (BHN)

4. Nani aliyefanya yote haya yatendeke?Ni nani aliyepanga wakati wa kila tukio?Mimi Mwenyezi-Mungu nipo tangu mwanzo,mimi nitakuwapo hata milele.

5. “Wakazi wa mbali wameona niliyotenda, wakaogopa;dunia yote inatetemeka kwa hofu.Watu wote wamekusanyika, wakaja.

6. Kila mmoja anamhimiza mwenzake akisema,‘Haya! Jipe moyo!’

7. Fundi anamhimiza mfua dhahabu,naye alainishaye sanamu kwa nyundo,anamhimiza anayeiunga kwa misumari.Wote wanasema, ‘Imeungika vizuri sana!’Kisha wanaifunga kwa misumari isitikisike.

8. “Sikiliza ewe Israeli, mtumishi wangu,wewe, Yakobo ambaye nimekuchagua,wewe mzawa wa Abrahamu, rafiki yangu;

9. wewe niliyekuleta toka miisho ya dunia,wewe niliyekuambia: ‘Wewe u mtumishi wangu;mimi sikukutupa, bali nilikuchagua.’

10. Basi, usiogope, mimi nipo pamoja nawe.Usifadhaike, mimi ni Mungu wako.Nitakuimarisha na kukusaidia;nitakulinda kwa mkono wangu wa ushindi.

11. “Naam! Wote waliokuwakia hasira,wataaibishwa na kupata fedheha.Wote wanaopingana nawe,watakuwa si kitu na kuangamia.

Kusoma sura kamili Isaya 41