Agano la Kale

Agano Jipya

Isaya 41:1-5 Biblia Habari Njema (BHN)

1. Mungu asema hivi:“Enyi wakazi wa mbali nyamazeni mnisikilize!Enyi mataifa jipeni nguvu;jitokezeni mkatoe hoja zenu,na tuje pamoja kwa hukumu.

2. “Nani, ila mimi, aliyemwita shujaa toka mashariki,mtu ambaye hupata ushindi popote aendako?Mimi huyatia mataifa makuchani mwake,naye huwaponda wafalme chini ya miguu yake!Upanga wake huwafanya kuwa kama vumbi,kwa upinde wake huwapeperusha kama makapi.

3. Yeye huwafuatia na kupita salama;huenda kasi kana kwamba hagusi chini.

4. Nani aliyefanya yote haya yatendeke?Ni nani aliyepanga wakati wa kila tukio?Mimi Mwenyezi-Mungu nipo tangu mwanzo,mimi nitakuwapo hata milele.

5. “Wakazi wa mbali wameona niliyotenda, wakaogopa;dunia yote inatetemeka kwa hofu.Watu wote wamekusanyika, wakaja.

Kusoma sura kamili Isaya 41