16. “Ee Bwana, Sisi twaishi kutokana na yote uliyotenda,kwa hayo yote mimi binafsi pia ninaishi.Nirudishie afya, uniwezeshe kuishi.
17. Nilipata mateso makali kwa faida yangu;lakini umeyaokoa maisha yangukutoka shimo la uharibifu,maana umezitupa dhambi zangu nyuma yako.
18. Huko kuzimu mtu hawezi kukushukuru wewe;waliokufa hawawezi kukushukuru wewe.Wala washukao huko shimonihawawezi tena kutumainia uaminifu wako.
19. Walio hai ndio wanaokushukuru,kama na mimi ninavyofanya leo.Kina baba huwajulisha watoto wao uaminifu wako.
20. “Mwenyezi-Mungu ataniokoa.Nasi tutamsifu kwa nyimbo za vinubisiku zote za maisha yetu,nyumbani kwake Mwenyezi-Mungu.”