Agano la Kale

Agano Jipya

Isaya 38:16-20 Biblia Habari Njema (BHN)

16. “Ee Bwana, Sisi twaishi kutokana na yote uliyotenda,kwa hayo yote mimi binafsi pia ninaishi.Nirudishie afya, uniwezeshe kuishi.

17. Nilipata mateso makali kwa faida yangu;lakini umeyaokoa maisha yangukutoka shimo la uharibifu,maana umezitupa dhambi zangu nyuma yako.

18. Huko kuzimu mtu hawezi kukushukuru wewe;waliokufa hawawezi kukushukuru wewe.Wala washukao huko shimonihawawezi tena kutumainia uaminifu wako.

19. Walio hai ndio wanaokushukuru,kama na mimi ninavyofanya leo.Kina baba huwajulisha watoto wao uaminifu wako.

20. “Mwenyezi-Mungu ataniokoa.Nasi tutamsifu kwa nyimbo za vinubisiku zote za maisha yetu,nyumbani kwake Mwenyezi-Mungu.”

Kusoma sura kamili Isaya 38