Agano la Kale

Agano Jipya

Isaya 37:23-38 Biblia Habari Njema (BHN)

23. Wewe umemtukana nani?Umemkashifu nani?Umethubutu kumbeza nani kwa majivuno?Ni mimi Mungu, Mtakatifu wa Israeli!

24. Umewatumia watumishi wako kunidhihaki mimi Bwana;wewe umesema, ‘Kwa magari yangu mengi ya vita,nimekwea vilele vya milima,mpaka kilele cha Lebanoni.Nimeangusha mierezi yake mirefu,na misonobari mizurimizuri.Nimevifikia vilele vyakena ndani ya misitu yake mikubwa.

25. Nimechimba visima na kunywa maji yake,na nilikausha vijito vya Misrikwa nyayo za miguu yangu.’

26. “Je, hujasikia ewe Senakeribu kwambanilipanga jambo hili tangu zamani?Ninachotekeleza sasa nilikipanga zamani.Nilikuweka uifanye miji yenye ngomekuwa rundo la magofu.

27. Wakazi wake wakiwa wameishiwa nguvu,wametishika na kufadhaika.Wamekuwa kama mimea shambani,kama nyasi changa shambani,kama majani yaotayo juu ya paaau kama ngano kabla hazijakomaaambazo hunyauka upepo mkavu uvumapo.

28. Lakini, nakujua wewe Senakeribu;najua kila unachofanya na kuacha kufanya;najua mipango yako dhidi yangu.

29. Kwa vile umefanya mipango dhidi yanguna nimeusikia ufidhuli wako,nitatia ndoana yangu puani mwako,na lijamu yangu kinywani mwako.Nitakurudisha njia ileile uliyojia.”

30. “Na hii ndiyo itakuwa ishara kwako Hezekia: Mwaka huu na mwaka ujao mtakula kinachomea chenyewe bila kupandwa. Lakini katika mwaka wa tatu mtapanda na kuvuna mavuno; mtapanda mizabibu na kula matunda yake.

31. Wale watakaobaki katika ukoo wa Yuda wataongezeka na kuwa wengi kama vile mti unavyotoa mizizi yake udongoni na kuzaa matunda juu.

32. Maana kutakuwa na watu watakaosalia huko Yerusalemu; naam, huko mlimani Siyoni kutakuwako watu wachache watakaosalimika.” Mwenyezi-Mungu wa majeshi amedhamiria kukamilisha hayo.

33. Mwenyezi-Mungu asema hivi juu ya mfalme wa Ashuru: “Hataingia katika mji huu, wala kuupiga mshale wala kuingia kwa ngao wala kuuzingira.

34. Atarudi kwa njia ileile aliyojia na wala hataingia katika mji huu. Mimi Mwenyezi-Mungu nimetamka hayo.

35. Naam, kwa ajili ya heshima yangu mimi na kwa ajili ya mtumishi wangu Daudi nitaulinda na kuuokoa mji huu.”

36. Basi, wakati wa usiku malaika wa Mwenyezi-Mungu aliingia kambini mwa Waashuru na kuwaua watu 185,000. Halafu kulipopambazuka watu hao wote walionekana wakiwa maiti.

37. Kisha Senakeribu mfalme wa Ashuru akaondoka, akaenda kwake, akakaa Ninewi.

38. Siku moja, wakati Senakeribu alipokuwa akiabudu katika nyumba ya Nisroki mungu wake, wanawe wawili, Adrameleki na Sharezeri, walimuua kwa upanga, halafu wakakimbilia nchini Ararati. Naye Esar-hadoni, mwanawe, akatawala badala yake.

Kusoma sura kamili Isaya 37