1. Karibieni mkasikilize enyi mataifa,tegeni sikio enyi watu.Sikiliza ee dunia na vyote vilivyomo,ulimwengu na vyote vitokavyo humo!
2. Mwenyezi-Mungu ameyakasirikia mataifa yote,ameghadhabika dhidi ya majeshi yao yote.Ameyapangia mwisho wao,ameyatoa yaangamizwe.
3. Maiti zao zitatupwa nje;harufu ya maiti zao itasambaa;milima itatiririka damu yao.
4. Jeshi lote la angani litaharibika,anga zitakunjamana kama karatasi.Jeshi lake lote litanyauka,kama majani ya mzabibu yanyaukavyo,naam, kama tunda la mtini linyaukavyo.