8. Barabara kuu zimebaki tupu;hamna anayesafiri kupitia humo.Mikataba inavunjwa ovyo,mashahidi wanadharauliwa.Hamna anayejali tena maisha ya binadamu.
9. Nchi inaomboleza na kunyauka;misitu ya Lebanoni imekauka,bonde zuri la Sharoni limekuwa jangwa,huko Bashani na mlimani Karmelimiti imepukutika majani yake.
10. Mwenyezi-Mungu asema hivi:“Sasa mimi nitainuka;sasa nitajiweka tayari;sasa mimi nitatukuzwa.
11. Mipango yenu yote ni kama makapi,na matokeo yake ni takataka tupu.Pumzi yangu itawaangamiza kama moto.
12. Watu watakuwa kama wamechomwa kuwa majivu,kama miiba iliyokatwa na kuteketezwa motoni.
13. Sikilizeni mambo mliyofanya enyi mlio mbali,nanyi mlio karibu kirini uwezo wangu.”