Agano la Kale

Agano Jipya

Isaya 33:6-12 Biblia Habari Njema (BHN)

6. Enyi watu wa Yerusalemu,Mwenyezi-Mungu atawajalieni usalama,atawaokoa na kuwapa hekima na maarifa.Hazina yenu kuu ni kumcha Mwenyezi-Mungu.

7. Haya, mashujaa wao wanalia,wajumbe wa amani wanaomboleza.

8. Barabara kuu zimebaki tupu;hamna anayesafiri kupitia humo.Mikataba inavunjwa ovyo,mashahidi wanadharauliwa.Hamna anayejali tena maisha ya binadamu.

9. Nchi inaomboleza na kunyauka;misitu ya Lebanoni imekauka,bonde zuri la Sharoni limekuwa jangwa,huko Bashani na mlimani Karmelimiti imepukutika majani yake.

10. Mwenyezi-Mungu asema hivi:“Sasa mimi nitainuka;sasa nitajiweka tayari;sasa mimi nitatukuzwa.

11. Mipango yenu yote ni kama makapi,na matokeo yake ni takataka tupu.Pumzi yangu itawaangamiza kama moto.

12. Watu watakuwa kama wamechomwa kuwa majivu,kama miiba iliyokatwa na kuteketezwa motoni.

Kusoma sura kamili Isaya 33