Agano la Kale

Agano Jipya

Isaya 33:2-7 Biblia Habari Njema (BHN)

2. Ee Mwenyezi-Mungu, utuonee huruma,kwako tumeliweka tumaini letu.Uwe kinga yetu kila siku,wokovu wetu wakati wa taabu.

3. Kwa kishindo cha sauti yako watu hukimbia;unapoinuka tu, mataifa hutawanyika.

4. Maadui zao wanakusanya mateka,wanayarukia kama panzi.

5. Mwenyezi-Mungu ametukuka,yeye anaishi juu mbinguni.Ameujaza Siyoni haki na uadilifu.

6. Enyi watu wa Yerusalemu,Mwenyezi-Mungu atawajalieni usalama,atawaokoa na kuwapa hekima na maarifa.Hazina yenu kuu ni kumcha Mwenyezi-Mungu.

7. Haya, mashujaa wao wanalia,wajumbe wa amani wanaomboleza.

Kusoma sura kamili Isaya 33