2. Ee Mwenyezi-Mungu, utuonee huruma,kwako tumeliweka tumaini letu.Uwe kinga yetu kila siku,wokovu wetu wakati wa taabu.
3. Kwa kishindo cha sauti yako watu hukimbia;unapoinuka tu, mataifa hutawanyika.
4. Maadui zao wanakusanya mateka,wanayarukia kama panzi.
5. Mwenyezi-Mungu ametukuka,yeye anaishi juu mbinguni.Ameujaza Siyoni haki na uadilifu.
6. Enyi watu wa Yerusalemu,Mwenyezi-Mungu atawajalieni usalama,atawaokoa na kuwapa hekima na maarifa.Hazina yenu kuu ni kumcha Mwenyezi-Mungu.
7. Haya, mashujaa wao wanalia,wajumbe wa amani wanaomboleza.