Agano la Kale

Agano Jipya

Isaya 33:19-24 Biblia Habari Njema (BHN)

19. Hamtawaona tena watu wale wenye kiburi,wanaozungumza lugha isiyoeleweka.

20. Tazameni Siyoni tunamofanya sikukuu zetu;tazameni mji Yerusalemu, makao matulivu, hema imara;vigingi vyake havitangolewa kamwe,kamba zake hazitakatwa hata moja.

21. Humo Mwenyezi-Mungu atatuonesha ukuu wake.Kutakuwa na mito mikubwa na vijito,ambamo meli za vita hazitapita,wala meli kubwa kuingia.

22. Maana Mwenyezi-Mungu ni hakimu wetu,yeye ni mtawala wetu;Mwenyezi-Mungu ni mfalme wetu,yeye ndiye anayetuokoa.

23. Ewe Siyoni, kamba zako zimelegea,haziwezi kushikilia matanga yake,wala kuyatandaza.Lakini nyara nyingi zitagawanywa;hata vilema wataweza kuchukua sehemu yao.

24. Hakuna atakayesema tena ni mgonjwa;watu watasamehewa uovu wao wote.

Kusoma sura kamili Isaya 33