Agano la Kale

Agano Jipya

Isaya 31:1-7 Biblia Habari Njema (BHN)

1. Ole wao wale waendao Misri kuomba msaada,ole wao wanaotegemea farasi,wanaotegemea wingi wa magari yao ya vita,na nguvu za askari wao wapandafarasi,nao hawamtegemei Mtakatifu wa Israeli,wala hawamwombi Mwenyezi-Mungu shauri!

2. Mungu ni mwenye busara na huleta maangamizi.Habadilishi tamko lake;ila yuko tayari kuwakabili watu waovukadhalika na wasaidizi wa watendao mabaya.

3. Wamisri ni binadamu tu wala si Mungu;farasi wao nao ni wanyama tu, si roho.Mwenyezi-Mungu akiunyosha mkono wake,taifa linalotoa msaada litajikwaa,na lile linalosaidiwa litaanguka;yote mawili yataangamia pamoja.

4. Mwenyezi-Mungu aliniambia:“Kama vile simba au mwanasimba angurumavyokuyakinga mawindo yake,hata kundi la wachungaji likiitwa kumkabili,yeye hatishiki kwa kelele zao,wala hashtuki kwa sauti zao.Ndivyo atakavyoshuka Mwenyezi-Mungu wa majeshikupigana juu ya mlima Siyoni na kilima chake.

5. Kama ndege arukavyo juu ya viota vyake,ndivyo Mwenyezi-Mungu atakavyoulinda Yerusalemu,ataulinda na kuukomboa,atauhifadhi na kuuokoa.

6. Enyi Waisraeli,mrudieni huyo mliyemsaliti vibaya.

7. Wakati utafika ambapo nyotemtavitupilia mbali vinyago vyenuvya fedha na dhahabu ambavyommejitengenezea kwa mikono yenu,vikawakosesha.

Kusoma sura kamili Isaya 31