Agano la Kale

Agano Jipya

Isaya 27:6-13 Biblia Habari Njema (BHN)

6. Itakuja siku wazawa wa Yakobo watashika mizizi;naam, watu wa Israeli watachanua na kuchipua,na kuijaza dunia yote kwa matunda.

7. Mungu hakuwaadhibu Waisraeli vikalikama alivyowaadhibu maadui wake;Waisraeli waliopotea vitani,ni wachache kuliko wale wa maadui zake.

8. Aliwaadhibu watu wake kwa kuwapeleka uhamishoni.Wakati wa upepo mkali wa mashariki,aliwaondoa kwa kipigo kikali.

9. Hivi ndivyo uovu wa wazawa wa Yakobo utakavyoondolewa,hivi ndivyo dhambi yake itakavyofutwa kabisa:Ataziharibu madhabahu za miungu;mawe yake yatasagwasagwa kama chokaa;Ashera, wala madhabahu za kufukizia ubani hazitabaki.

10. Mji ule wa ngome sasa umekuwa mtupu,umeachwa na kuhamwa kama jangwa,humo ndama wanalisha na kupumzika.

11. Matawi ya miti yamekauka na kuvunjika;kina mama huyaokota wakawashia moto.Watu hawa hawajaelewa kitu,kwa hiyo Mungu, Muumba wao, hatawahurumia,yeye aliyewafanya, hatawafadhili.

12. Siku hiyo, kutoka mto Eufrate hadi mpakani mwa Misri, Mwenyezi-Mungu ataipura nafaka yake, nanyi Waisraeli mtakusanywa mmojammoja.

13. Siku hiyo, tarumbeta kubwa itapigwa na watu wote wa Israeli waliopotea nchini Ashuru au waliotawanywa nchini Misri watarudi na kumwabudu Mwenyezi-Mungu juu ya mlima mtakatifu huko Yerusalemu.

Kusoma sura kamili Isaya 27