1. Siku hiyo, Mwenyezi-Mungu atautwaa upanga wake mkubwa, mkali na imara, na kuliadhibu dude Lewiyathani joka lirukalo na danganyifu; Mwenyezi-Mungu ataliua joka liishilo baharini.
2. Siku hiyo, Mwenyezi-Mungu atasema hivi:“Imbeni utenzi wa shamba langu zuri la mizabibu!
3. Mimi, Mwenyezi-Mungu, ni mkulima wake;nalimwagilia maji kila wakati,ninalilinda usiku na mchana,lisije likaharibiwa na mtu yeyote.
4. Silikasirikii tena shamba hili;kama miiba na mbigili ingelilivamia,mimi ningepambana nayo na kuichoma moto.