Agano la Kale

Agano Jipya

Isaya 2:9-21 Biblia Habari Njema (BHN)

9. Kwa hiyo, kila mtu ataaibishwa na kufedheheshwa.Usiwasamehe hata kidogo, ee Mungu!

10. Ingieni katika mwamba,mkajifiche mavumbini,kuiepa hasira ya Mwenyezi-Mungu,mbali na utukufu wa enzi yake.

11. Siku yaja ambapo kiburi cha watu kitashushwa,majivuno ya kila mtu yatavunjwa;na Mwenyezi-Mungu peke yake atatukuzwa siku hiyo.

12. Naam, yaja siku ya Mwenyezi-Mungu wa majeshidhidi ya wenye kiburi na majivuno,dhidi ya wote wanaojikweza;

13. dhidi ya mierezi yote ya Lebanoni,ambayo ni mirefu na mizuri,dhidi ya mialoni yote nchini Bashani;

14. dhidi ya milima yote mirefu,dhidi ya vilima vyote vya juu;

15. dhidi ya minara yote mirefu,dhidi ya kuta zote za ngome;

16. dhidi ya meli zote za Tarshishi,na dhidi ya meli zote nzuri.

17. Kiburi chote cha watu kitakomeshwa,majivuno ya kila mtu yatavunjwa.Na Mwenyezi-Mungu peke yake atatukuzwa siku hiyo.

18. Vinyago vyote vya miungu vitatoweka kabisa.

19. Ingieni katika mapango miambani,katika mashimo ardhini,kuiepa hasira ya Mwenyezi-Mungu,mbali na utukufu wa enzi yake,atakapokuja kuitia hofu dunia.

20. Siku hiyo, watu watawatupia panya na popovinyago vyao vya fedha na dhahabuwalivyojitengenezea ili kuviabudu.

21. Nao wataingia katika mapango miambanina kwenye nyufa za miamba,kuiepa hasira ya Mwenyezi-Mungu,mbali na utukufu wa enzi yake,atakapokuja kuitia hofu dunia.

Kusoma sura kamili Isaya 2