Agano la Kale

Agano Jipya

Isaya 2:14-19 Biblia Habari Njema (BHN)

14. dhidi ya milima yote mirefu,dhidi ya vilima vyote vya juu;

15. dhidi ya minara yote mirefu,dhidi ya kuta zote za ngome;

16. dhidi ya meli zote za Tarshishi,na dhidi ya meli zote nzuri.

17. Kiburi chote cha watu kitakomeshwa,majivuno ya kila mtu yatavunjwa.Na Mwenyezi-Mungu peke yake atatukuzwa siku hiyo.

18. Vinyago vyote vya miungu vitatoweka kabisa.

19. Ingieni katika mapango miambani,katika mashimo ardhini,kuiepa hasira ya Mwenyezi-Mungu,mbali na utukufu wa enzi yake,atakapokuja kuitia hofu dunia.

Kusoma sura kamili Isaya 2